Jumatatu, 18 Mei 2015

MAKALA: Maisha ni Juhudi Binafsi!




Mafanikio ni juhudi binafsi.

Na Gabriel Manoko
O712708790
         Kuna wakati unakutana na mtu anakusimulia historia ya maisha yake na mafanikio ambayo kayapata unabaki umeduwaa, unaweza ukawa unashangaa lakini mwisho unaona manufaa ya kutumia vizuri akili ambazo tumepewa na mwenyezi Mungu, kufikiria na kufanyia kazi mambo yanayoweza kubadilisha maisha.
Kwangu huyu ninaweza kumuita msichana mwenye malengo ya mbali , ana akili pia anatumia maamuzi sahihi na busara kwa kuamini kuwa uthubutu wa kufanya jambo huleta mabadiliko makubwa ya maendeleo kwenye jamii na hata kwenye familia yake.
Huyu si mwingine, bali ni Suzana Raphael (22) msichana ambae kwa makala hii anaweza kuwa chachu ya wasichana wengine wa hapa kwetu Tanzania na hata nje ya nchi kwa kuona thamani ya kufanya swala zima la u modal na kuweza kujipatia kipato halali na kuweza kujipanga kuondokana na umasikini.
Suzana ni modal ambaye anafanya kazi na wanamitindo (Designers) mbalimbali kama Mustafa Hasanari na Hadija Mwanamboka, ambapo aliweza kuonyesha mavazi mbalimbali katika show tofauti tofauti kama Swahili fashion na Red in red ambazo zilifanyika mkoani Dar es salaam.
Historia ya elimu
Suzana ni mzaliwa wa Musoma na ni mtoto wa mwisho kuzaliwa katika familia ya watoto watatu, ambapo aliweza kumaliza darasa la saba mwaka (2004), na kuweza kuendelea na elimu ya kidato cha kwanza mwaka (2005). Na  alimaliza kidato cha nne mwaka (2008)katika shule ya Baptist Sekondari ambayo ipo Magomeni Mkoani Dar es Salaam.
Kuingia kwenye Umodal wa mavazi
“Baada ya kumaliza kidato cha nne kipindi kipindi yupo kidato cha pili katika shule ya sekondali ya Perfect Vision aliweza kushiriki mashindano mbalimbali ambayo yameandaliwa na shule ,”anasema.
Lengo la mashindano hayo ilikuwa ni kuwakalibisha wanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule hiyo ya Perfect Vision,” anasimulia Suzana
Kuna siku alikutana na Nancy Sumari maeneo ya Ubungo na ndipo aliambiwa na Nancy kuna shindano la Kisura ambalo linazaminiwa na Psi na usaili utafanyika Club Maisha ambayo ipo Dar es salaam maeneo ya Osterbay. Alifika kwenye ukumbi huo na aliweza kukutana na wadada wengi ambao walikuwa wanasubiri usahili na yeye alifanikiwa kushinda na kwenda kambini kwa ajili ya mashindano hayo. Waliweza kukaa kwenye hoteli ya Kiromo ambayo ipo Bagamoyo na waliweza kukaa huko kwa muda wa miezi mitano,” anasema Suzana
Aliweza kuingia kwenye fainali ya mashindano hayo ambayo yalifanyika katika hoteli ya Serena hiliyopo Dar es salaam, mshindi wa kwanza alikuwa Eliza na yeye alikuwa mshindi wa tatu na kuweza kupata msaada wa kwenda kusoma katika chuo cha urembo kinachoitwa PURE na kutokana na mashindano hayo ndipo wanamitindo (Designers) wakubwa wa hapa nchini kama Mustafa Hasanari na Hadija Mwanamboka  waliweza kumuona siku ya fainali na kuanza kufanya nae kazi ya Umodal.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni