Jumamosi, 23 Mei 2015

DHAMIRA CHOMOZI KATIKA RIWAYA YA BINA-ADAM



Madumulla (2009) anasema, riwaya ni nathari bunifu simulizi kama vile hadithi, hekaya na ngano inayosimuliwa kwa mdomo.Anaendelea kusema kuwa fasihi ilitokana na maandiko ya fani ya ushairi hususani tendi za kiswahili katika hati za kiarabu kwasababu ndio maandishi yaliyotamba katika pwani ya Afrika mashariki.
Pia, Muhando.P na Balisidya(1976)wasema, riwaya yaweza kuanzia maneno 35,000 na kuendelea, lakini tukisema juu ya urefu na kuishia hapo tu,jambo hili halitakuwa na maana. Maana mtu yeyote anaweza kuweka habari yoyote ile katika wingi wa maneno kama hayo.Jambo muhimu hapo ni kuwa riwaya huwa na mchangamano wa matukio,ujenzi wa wahusika, dhamira,muundo wake na hata mtindo.Mwandishi tuseme ana uwezo wa kutamba na kutambaa mahali pengi na kutambaa vizingiti kama apendavyo ili kujenga hadithi hiyo ndefu.
 Vilevile,Wamitila (2003) anasema, riwaya ni kazi ya kinathari au kibunilizi ambayo huwa na urefu wa kutosha, msuko uliojengeka vizuri,wahusika wengi walioendelezwa kwa kina wenye kuchukua muda mwingi katika maandalizi na kuhusisha mandhari maalum.
Sanjari na hao, Nkwera (1978) anasema, riwaya ni hadithi iliyo ndefu kuweza kutosha kufanya kitabu au zaidi. Ni hadithi ya kubuniwa iliyojengwa juu ya tukio la kihistoria au kuandikwa kwa mtindo wa ushairi au mfululizo wa kinaganaga katika uelezaji wa maisha ya mtu au watu na hata taifa.
Kwahiyo, tunaweza kusema kuwa riwaya ni kazi iliyoandikwa kwa mtindo wa kinathari ambayo ina urefu wa kiasi fulani,ni pana, ina uchangamano wa kimtindo na kidhamira na ina shughulikia masuala kadhaa katika mtazamo mpana wa wakati.Baaba ya kuangalia maana ya riwaya kutoka kwa waandishi mbalimbali zifuatazo ni sifa za riwaya kutoka kwa Madumila (2009) kama ifuatavyo;
Kwanza, huwa na urefu na upana wa kutosha, maranyingi huusisha upana wa kijografia inaweza kuchukua hata ulimwengu mzima. Kulingana na hali hiyo pia hufanya kupatikana dhamira nyingi sana kwa sababu huhusisha mambo mengi kijiografia.
Pili, riwaya haifungwi na sheria wala kanuni, utanzu huu huwa haufingwi na kanuni za uandishi kama tanzu zingine kama ushairi. Maranyingi utanzu wa ushairi huwa unakanuni zake za uandishi kama kufuata uandishi wa urari wa vina na mizani na lugha ya mkato.
Tatu, riwaya inauhitaji wa kusoma na kuandika, stadi hizi mbili huwa ni nguzo muhimu katika utanzu wa riwaya. Kwa hiyo riwaya haina nafasi kwa jamii ambayo haijui kusoma wala kuandika. Kwa hali hii utanzu kama ushairi inaweza kushughulikiwa hata na mtu ambaye hana taaluma ya kusoma na kuandika mfano, Haji Gora Haji ni mtaalamu wa mashairi lakini hana stadi za kusoma na kuandika.
Nne, riwaya huitaji uchumi madhubuti kwa sababu huiitaji viwanda kwa ajili ya kuchapa vitabu ili iwafikie walengwa. Kwa sababu riwaya huwa inaweza kuzungumzia mambo mengi katika ulimwengu mfano ubepari, utandawazi na ujasusi.
Baada ya kuangalia maana za riwaya na sifa mbalimbali za riwaya ifuatayo ni historia ya mtunzi na utunzi wake kwa mujibu wa Swahili foramu;
Kyllo W. W. alizaliwa mwaka 1966 mjini Machakos nchini Kenya ni mwandishi anayeandika katika tanzu za ushairi, tamthilia, hadithi fupi na riwaya. Pia ameandika vitabu kadhaa vya watoto. Hadi leo hii amechapisha riwaya tatu ambazo niNguvuyaSala (1999), BinaAdamu! (2002) na Musaleo (2005). Riwaya hizi zilikuwa na ubunifu sana wa kisanaa hadi zikafikia hatua za kushinda tunzo ya fasihi ya Jomo Kenyatta mnamo  mwaka 2001 na 2005. Pia ni mhakiki wa fasihi ambaye amechapisha makala mbalimbali katika majarida ya kiusomi Afrika, Ulaya na Marekani. Mwandishi ana shahada ya uzamifu(Phd) katika fasihi. Mwandishi huyu pia ameweza kutunga vitabu vingine kama vile; Wingulakupita (Tamthilia), kamusiyaMethali, kamusiyaMisemo na Nahaunauhakikiwafasihi. Mwandishi anasema alitumia mwaka mmoja kuiandika riwaya ya Bina –Adamu. Kwa sasa Wamitila ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi.
Bina – Adamu! ni riwaya iliyotumia sitiari ya kijiji kuangalia hali ya mataifa ya ulimwengu katika kipindi hiki ambapo hali za kijamii, kisiasa na kiuchumi zinadhibitiwa na ubepari wa mataifa yaliyoendelea. Hii niriwaya ambayo inaelezea mambo mbalimbali ambayo yanaendelea kutendwa na mataifa yalioendelea dhidi ya mataifa yanayoendelea yaliyo katika bara la Afrika. Riwaya ya Bina – Adamu! inaelezea mambo mbalimbali kama athari za ubepari kama vile, Afrika na uongozi wa mabavu. Mwandishi wa riwaya hii aliamua kutunga kazi hii ili kukemea utawala wa kibepari unaoendeshwa hadi leo hii na yanchi Marekani kwa mataifa yanayoendelea.Baada ya kuangalia historia ya mwandishi na utunzi wake ufuatayo ni uainishaji wa aina ya riwaya;
Kuna   ainakuumbilizariwaya ambazoniriwayadhatinariwayapendwa. Riwayahiiinaingiakatikaainayariwayadhati. Riwaya dhati ni riwaya zinazo jadili mambo nyeti yanayo tokea katika jamii. Hutumia lugha nyoofu na fasaha, hivyo riwaya hizi hazitumii lugha ya matusi.  Riwaya pendwa ni riwaya ambazo zinajadili masuala kama vile upelelezi, mapenzi, ujasusi na ujambazi. Katika riwaya pendwa fani huchomoza zaidi kuliko maudhui.
 Kwa kuzingatia kigezo cha fani, RiwayayaBina – Adamu!niriwaya changamani kwani,riwayachangamaniniriwayaambayohuhitajikusomwakwa makini ili msomaji aweze kuelewa. Aghalabuhuwanamaudhuimenginawahusikawengiambaowanachangiakatikakujengawazokuu la riwaya    hii. Hiinikwamujibu wa www.gafkosoft.com/swa/riwaya 2009-2014.
Piasifazariwayachangamanizimetufanyakusemariwayahiinichangamanikwaniriwaya changamanimaudhuiyakeyanatakiwakutafakarizaidiilikupatakilekilichokusudiwa. Lichayasifahiyo, riwayachangamanihutumialughayamafumbozaidi.Sifahizizimeonekanakwakiasikikubwakatikariwayahii, nasifahizondizozikafanyatuiwekekatikakundi la riwayachangamani.
Kwakuthibitisha haya,mwandishiametumialughayamafumbokwakiasikikubwakatikakaziyake. Kwanihajatajamojakwamojahadhira yake anayoiandikialakinikwakupitia mafumbonataswirazilizotumikaunawezakubashirimaeneonamazingirayanayozungumziwakatikariwayahii. Mfano(uk.100), mwandishiametumialughayamafumbokuwarejeleawazeewalivyopambanakatikakipindi cha harakatizaukombozi.Mwandishianasema,
“Wazeewalinielezamatatizomengiwaliyokabiliananayozamaniwalipokuwa wakipambananamazimwiyaliyoivamianyumbamiakamingiiliyopita.”
Mwandishiametumiapichayamazimwikurejeleawakolonina nchizakiafrikazilizovamiwakatikakipindi cha utawalawakikoloni.
Piakatikakuendeleakuthibitishakuwahiiniriwayachangamani mtunzi ametumiataharukikatikauelezeajiwamatukio,hii ni kuwafanyahadhira wake waendeleekuisomailikujuaninialikuwaamelengakuwasilishakwahadhira. Imejitokezakatikasuraya kwanza yariwayaambapo msomajiakisomasuramojahataelewaninimwandishiamelengakuelezeaisipokuwahadimsomajiaendeleekusomasurazingineilikuunganishamatukionakupatamadhui hii.
Baada ya kujadili uainishaji wa riwaya zifuatazo ni dhamira chomozizilizojadiliwa na mwandishi katika riwaya ya Bina – Adamu!;
Utabaka, ni hali ya kuwepo na tofauti za kimaisha miongoni mwa wanajamii. Tofauti hizo zinaweza kuwa za kiuchumi, kisiasa na kadharika. Katika riwaya ya Bina - Adamu! mwandishi ameonyesha matabaka ya kiuchumi, kisiasa na kijamii yanayojitokeza katika jamii.Mfano, katika (uk. 67) mwandishi anasema,
“Nyumba nyingi zimeinamiwa na miti mbalimbali ya matunda; miembe, mipapai,         michungwa, mikakao, mipira, minazi… Kila kiongozi amekaa huko juu paani, huko ndiko anakochumia matunda kwa rahisi na kuwatupia watu walioko chini ambao wameshikia ngazi ya kupanda juu. Lakini kuna wengine ambao wanachofanya ni kula wakashiba kwanza kisha kuyatupa makaka, makokwa na maganda huko chini yanakogang’ang’aniwa na umati mkubwa ulioko huko.”
Hapa mwandishi anazisawili nchi nyingi za Afrika kwakuonyesa matabaka ya kisiasa yaliyopo kati ya jamii na viongozi wao. Viongozi wengi wa Afrika hula na kushiba ndipo huwakumbuka wananchi wake ambao ndiyo wameshikilia ngazi hiyo ambayo wamepanda.
Mwandishi anazidi kuonyesha utabaka wa kisiasa katika jamii ambapo viongozi ambao ndiyo wameshikilia madaraka jinsi wanavyohamishamalighafi za wanajamii na kuzihamishia nje ya nchi kwa manufaa yao binafsi. Anasema katika (uk. 67),
“Wengine wanaiba na kuhamishia kwingine, labda ughaibuni.”
Pia mwandishi anazidi kuonyesha matabaka yanayotokea katika jamii, kuna tabaka la juu tabaka la kati na tabaka la chini. Tabaka la juu linaposhiba huwarushia tabaka la kati, na tabakala katilinaposhiba hurushia tabaka la chini ambalo ni wananchi. Mwandishi anaonyesha katika (uk. 69) anaposema,
“Nilimwangalia yule mtu aliyeketi jukwaani. Ni kweli alikuwa akila matunda aliyokuwa akitunda kwenda kwenye mti uliokuwa umeiinamia nyumba hiyo. Mengine aliyatupia jamaa waliokuwa kwenye sehemu ya chini karibu na ukingo wa ngazi ya kupandia paani. Wasiyoyataka waliyatupia nyuma yakaangukia umati mkubwa ulikuwa huko chini. Umati mwenyewe umekodoa macho pima huko juu kama kuu anayemwangalia mwewe.”
Vilevile, mwandishi ameonyesha matabaka ya kiuchumi katika riwaya ya Bina-Adamu!,ambapo jinsi viongozi wa ngazi za juu wanavyofuja pesa za umma na kuwaacha viongozi wa ngazi ya chini na hata wananchi wakiwa na hali mbaya ya kiuchumi. Hii imejidhihirisha katika (uk. 111) anasema,
“… Nilikumbuka kisa kilichotokea siku fulani katika nchi yangu. Kuna wakati serikali ilipofuja pesa kununua magari mengi ajabu kwa kuwa kulikuwa na mkutano fulani wa viongozi wa nchi huru barani. Baada ya mkutanohuo, magari hayo yalipewa marafiki wa viongozi. Siwezi kusahau hili kwa kuwa siku hizo, tulikuwa tukisoma na mkaguzi wa elimu wa wilaya alikuwa akitembelea shule za kwetu kwa baiskeli.”
Mapambano dhidi ya ukoloni, huonyesha jinsi jamii ilivyopambana dhidi ya ukoloni ili kijikomboa na kupata uhuru. Katika riwaya ya Bina-Adamu mwandishi ameonyesha jinsi wazee walivyopambana katika kuuondoa ukoloni. Hii inajitokeza katika (uk. 100) anasema,
“Wazee walinieleza matatizo mengi waliyokabiliana nayo zamani walipokuwa wanapambana na mazimwi yaliyovamia nyumba miaka mingi iliytopita,“Ilitubidi kuzitumia ala zozote tulizokuwa nazo; majembe, miundu, hanjari, mishale, na kila kitu tuseme. Lakini hatimaye tulifanikiwa, alieleza mzee mmoja usiku tukifurahia mbalamwezi”
Mwandishi ametumia lugha ya picha ya Mazimwi akimanisha ‘Wakoloni’. Dhamira hii inasawiri nchi za Afrika zilizokuwa zimetawaliwa na wakoloni na jinsi walivyopigana hadi kupata uhuru wao.
Historia na uhistoria, dhamira za kihistoria zinalenga kuelezea mapito ambayo watu wamepitia. Mfano; kabla ya ukoloni, harakati za ukombozi na hata baada ya uhuru. Kabla ya ukombozi kazi nyingi zililenga kuwahimiza watu wajikomboe kwa kueleza mabaya yaliyofanywa na wakoloni na baada ya uhuru zilihimizakujenga jamii mpya. Dhamira hii ya historia na uhistoria imejitokeza katika riwaya hii ya Bina – Adamu ambapo, mwandishi anaelezea jinsi jamii zilivyopambana na ukoloni mpaka kuwaondoa wakoloni na hatimaye kupata uhuru. Mwandishi anazidi kuelezea jinsi viongozi walioaminiwa na kuchaguliwa kuingia kwenye utawala baada ya ukoloni jinsi walivyowasaliti wananchi. Anasema katika uk. 100
“Wazee walinieleza matatizo mengi waliyokabiliana nayo zamani walipokuwa wanapambana na mazimwi yaliyovamia nyumba miaka mingi iliytopita”.
“Ilitubidi kuzitumia ala zozote tulizokuwa nazo; majembe, miundu, hanjari, mishale, na kila kiyu tuseme. Lakini hatimaye tulifanikiwa,” alieleza mzee mmoja mmoja usiku tukifurahia mbalamwezi.
“Hatimaye tulifanikiwa kisha kikaja kipindi cha ahadi za wenzetu waliokuwa na nguvu
za kuuongoza ukoo, tukawaamini. Kumbe ni kosa kubwa tulilolifanya.” Walieleza
matatizo waliyoyapata siku hizi; Karo ya watoto, upungufu wa chakula, magonjwa,
matatizo ya kazi….”                                                                                     
Hii dhamira ya historia na uhistoria inasawiri nchi za kiafrika ikiwemo Tanzania kabla na baada ya uhuru. Lengo la mwandishi ni kuwaamsha watu ili waweze kujenga jamii mpya ambayo haina matatizo kama hayo.
Utu na maadili, dhamira hii ni pana kwani wapo wanaojadili maadili katika wigo wa kisiasa na kidini dhamira ya utu na maadili huusisha vitu kama uchoyo, wizi, na ubinafsi. Katika riwaya ya BinaAdamumwandishi ameonyesha kuwa baadhi ya viongozi hawana maadili ya uongozi kama mwandishi anavyosema (uk. 91),
“… mamanchi alipomuuliza akambaka na kumuua. Ndugu yetu kabisa. Kakwea juu matunda anakula yeye tu na wenzake wachache, wezi wote! Wanaiba hata mbegu …”
Mwandishi anaonyesha jinsi viongozi wanavyoiba rasilimali za nchi bila kubakiza kitu. Vilevile mwandishi ameonyesha jinsi watalii (wageni) wanavyoharibu maadili ya jamii husika pale wanapokwenda kinyume na mila na desturi za jamii husika mwandishi ameyaonyesha haya katika (uk. 109) anaposema,
“… sikuwa na hakika kama alikuwa akinicheka mimi au akimcheka mtalii aliyekuwa amevua maguo yake na aliyekuwa akikimbia mbele za wenzake huku tumbo lake kubwa ajabu likichezacheza kama dodoki.”
Dhamira hii ikilinganishwa na maadili ya jamii za waafrika hususani Tanzania inaonyesha kuwa mtu huyo hakuwa na maadili katika muktadha wa jamii husika (watanzania) kwani kutembea tumbo nje nikinyume cha mila na desturi za watanzania.
 Uongozi na uwajibikaji, kuna viongozi ambao hawawasaidii wananchi wake kwa matatizo yanayotokea katika jamii. Viongozi kwenda kinyume na matakwa ya wananchi wao kwa kukiuka ahadi walizoziweka kwa wananchi wao, mfano katika (uk. 144) anasema,
“Nilikumbuka wanasiasa wa kwetu ambao hawachukui hatua yoyote au kufanya jambo bilaKukumbushwa.”
 Viongozi wengi katika jamii wakiona matatizo hawachukui hatua ya kuyatatua mpaka maafa na matatizo makubwa yanapotokea.Vilevile viongozi wengi wanatumia pesa za umma vibaya kwani wanafuja mali bila sababu ya msingi. Badala ya kutumia katika kuleta vitu vya maendeleo, vilevile hutumia pesa nyingi sana kwa kufanyia vitu visivyokuwa na maendeleo katika jamii mfano katika (uk. 111) tunaona viongozi wanavyofuja mali ya serikali bila msingi,anasema,
“nilikumbuka kisa kilichotokea siku fulani katika nchi yangu,kuna wakati serikali ilipofuja pesa kununua magari mengi ajabu kwa kuwa kulikua na mkutano fulani wa viongozi wa nchi huru barani. Baada ya mkutano huo,magari hayo yalipewa marafiki wa viongozi. Siwezi kusahau hili kwa kuwa siku hizo tulikua tukisoma na mkaguzi wa elimu wa Wilaya alikua akitembelea shule za kwetu kwa baiskeli.”
Vilevile viongozi wanatoa ahadi za uongo na kuwasaliti wananchi, katika (uk. 136) mwandishi anasema,
 Tulipopata uhuru tuliahidiwa kupata mashamba yaliyokua yamemilikiwa na
wenzangu.Uhuru ulikuja,lakini tuliendelea kulima vikataa vyetu visivyokua na
rutuba.Viongozi ndio wanayolima hayo mashamba.”
Dhamira hii inasawiri maisha ya waafrika kwani viongozi wengi ni wasaliti,wanafujaji pesa za umma kwakufanya kumbukizi kwa kutumia  gharama kubwa,badala yakufanya mambo ya kimaendeleo. Pia viongozi hawana utayari wa kutatua matatizo ya wananchi, mfano mzuri nchi  ya Kenya kuna sikukuu za kumbukizi kama Jomo Kenyatta na Tanzania siku ya Mwalimu Nyerere, Karume na sikukuu ya Muungano hadi kufikia hatua ya kutokutoa pesa za mikopo ya Elimu ya juu na mishahara kwa watumishi wa umma kama Walimu na Maaskari.
Ukoloni mamboleo,ni hali ya taifa moja kutawala taifa lingine kiuchumi,kifikra na kiutamaduni. Mataifa yaliyoendelea hutawala mataifa yanayoendelea kama Tanzania, Kenya, Uganda na Ruwanda katika nyanja zote hizo, mfano katika (uk.88) mwandishi ameonyesha ubaya wa wawekezaji kwa kusema;
…wamemwaga mafuta hapa samaki wafe wapate sababu ya kutuletea makopo.
Huku juuwanatupa mabaki ya nyuklia.”
Hapa tunaona kuwa mataifa yaliyoendelea wanavyoharibu malighafi za mataifa yanayoendelea ili wapate kuongeza soko kwa kuuza bidhaa zao. Vilevilemwandishi anaonyesha jinsi nchi za mataifa yaliyoendeleawanavyowafanyia majaribio ya kisayansi katika nchi zinazoendelea kama za kiafrika (uk.125),
 wali..ge..uzwa…vitu vya kufanyia..majaribio”
…”ya nini”Niliuliza kwa mshangao mkubwa.
“kua…ngali…a…a..ma..t.oke…o ya kaswende…katika mi..ili ya bin Adam.”
Vilevile mwandishi anaendelea kuonyesha jinsi ukoloni mamboleo ulivyoshamiri katika nchi za kiafrika, mfano katika (uk. 86) anaonyesha jinsi kituo cha elimu kilivyofungwa baada ya amrikutolewa na nchi zilizoendelea.
 kilikua kituo cha usomi hiki lakini alisema kifungwe.
 “ Nani?”                      
…hawakutaka kiendelee na utafiti wake wa kuifunua historia kwa kila mtu…”
Hapa tunaona kuwa mataifa yaliyoendelea hawataki nchi zilizokua chini yao waweze kujitambua  kwani wanaweza kujikomboa kutoka katika ukoloni mamboleo. Ukoloni mamboleo ni dhamira inayosawiri maisha halisi ya nchi za kiafrika kwani ukoloni umeshamiri sana nchi za kiafrika. Kwamfano, nchini Tanzania watoto wa shule za msingi hupewa chanjo kila mara na kusemekana kuwa ni majaribio ya kutibu ugonjwa fulani.
 Athari za utandawazi,utandawazi ni hali ya dunia kuonekana kama kijiji kimoja, kunakua na uhuru wa watu kusafiri kutoka sehemu moja na nyingine duniani, pamoja na uhuru wa kufanya biashara. Mwandishiameonesha athari za utandawazikama ifuatavyo;kwanza mipaka kufutwa na tamaduni za dunia kuingiliana, mfano katika (uk. 140) inaonesha,
mipaka mingi imefutwa,tamaduni sasa zinaingiliana na sisi tumewatangulia wengi
kwauchunguzi hata kuliko wenyewe.!”                                                                                              
Pili ni soko huria, utandawazi unasababisha soko huria duniani yaani taifa lolote duniani kuwa na uhuru wa kuuza na kununua bidhaa yoyote duniani,na madhara yake mataifa yaliyoendelea kukua kiuchumi kwa kuwa na soko kubwa nchi nyingine, mfano (uk. 146) anasema,
 kwani….haowanafanya shughuli zao ni nani?
 “wanasafirisha dhana za vita kwenda kuuza.”
         “wanawauzia nani?”
“sijui lakini nasikia kuna familia kadhaa wanagombana na hawa wanaamini  karibuni
 wanawanapigana.Wanataka kuliwahi soko.”
Hii inasawiri maisha ya Afrika kwani nchi nyingi za Afrika wanauziwa bidhaa za vita hata kama hamna vita.
Ubinafsishaji ni dhamiranyingineambayoimejitokeza katika riwaya hii ya Bina- Adamu. Mwandishiameonyeshajinsiwananchi ambavyohawarusiwi kutumia vitu vyao kwakuwa sharia haziwaruhusukwanitayariviwandahivyovimeshabinafsishwa. Mfano, (uk. 5)
                        “Kunaninihapa ?”                                                          
                       “ Hikinikiwanda”
                       “ Chanini?”
                      “ Reconditioned cars”
                      “ Mnazitumia?”
                    “ Ahh, dekimasen? Haiwezekani asilani.Sheriazetuzinakataza
                      Matumiziyamagarihayo!”
Piakatikaukurasahuuunaonyeshajinsiubinafsishajiunavyofanyakazinakusababishawatukukatazwakufanya shughuliambazonihakiyaonahatawabinafsishaji wakajionawaondiowakuukwaniwanadirikihatakusemakamatutakataakubinafsishwa, baadhiyamisaadaitasitishwa. Hiiimethibitishwanamwandishi aliposema,
“Karibuni tutaanza kuwauzia samaki wabichi”
“Hawana samaki huko?”
“Wanao lakini hawana idhini ya kuwavua, sisi tunayo,
wanapatikana kwenye maji ya kimataifa; International
waters. Tuna wavua na kuwapakia kwenye makopo huko huko
majini. Wanawapenda sana hawa wa makopo. Kwao ndiyo
maendeleo hayo! Wakiyagomea na si misaada ya kiuchumi kwao
tunaizuia.”                                                                         
Pia suala la ushirikiano, mwandishi amelionyesha kwa kutumia mhusika Mimi kurejelea mambo ambayo walikuwa wakiyatenda enzi za utoto. Hii inamaanisha kabla ya utandawazi kuingia katika nchi zetu. Mwandishi katika (uk. 57) anasema,
“Siku hizo tulikuwa tukienda kufuga mifugo ya kijiji pamoja.
Hapakuwa na tofauti wala hatukuwazia wapi ni wapi,
Tuliwalishapamoja… na kumbuka kuwa hata siku hizo aliyekosa
miongoni mwetu aliweza kuadhibiwa na mzazi yeyote sio lazima
awe wake. Lakini mambo yalikuwa yamebadilika.”
Mwandishi ameyaonyesha hayo ili kuonyesha jamii jinsi ilivyoathiriwa na utandawazi na kuwafanya watoto wengi kuwa na viburi kwa watu wengine.
Kwa mujibu wa Florence L. V. (2013) anasema, matukio ya ajabuajabu (usihiri) ni natukio ya kiajabu ambayo si ya kawaida iwapo tutayaweka katika ulimwengu wa kawaida.Haya ni matukio ambayo ni kinyume na matukio ya kawaida yanayotarajiwa na binadamu wa kawaida.
Sifa za uhalisia ajabu, au matukio ya ajabu ajabu (usihiri) katika riwaya ya Bina – Adamu ni kama zifuatazo;
Kwanza, kuwepo kwa wahusika ambao si wakawaida. Katika riwaya ya Bina – Adamu kuna wahusika wa aina mbili, wahusika binadamu na wasio binadamu. Mfano wa wahusika ambao ni binadamu ni pamoja na mhusikaMimi, P.P, Mwanamke, Wanaume, Babu … wahusika ambao si binadamu ni pamoja na mhusika Joka, matendo yaliyowasilishwa na viumbe pamoja binadamu ambayo si matendo ya kawaida ndio hudhihirisha uwepo wa usihiri katika riwaya hii kwa mfano (uk. 19-20) mwandishi anaposema,
“… niliangalia lile joka huku nikirudi nyuma nyuma huku sauti imenikwama. Kwenye mgongo wake kulikuwa na maandishi: Vitas; labda hakuwa nyoka bali macho yalinicheza tu. Ghafla           nilimwona akinyionyirika haraka haraka nami nikarudi nyuma wanguwangu. Nilikanyaga sehemu laini iliyomeguka na kunitupa chini. Lazima lile joka lilifuatia.”
Vile vile mwandisha ametumia mhusika beberu katika kuwasilisha matendo ya ajabu katika (uk. 14) mhusika Mimi anasema,
“Nilikaribia lakini nikalazimika kurudi nyuma baada ya kuinusa harufu mbaya kama ya beberu. Lazima jitu hilo lilitambua na kijiegeza nyuma. Beberu! Beberu! Beberu! Nilijianbia akilini nikiliangalia beberu beberu beberu, linanuka beberuu!..Lilitoweka ghafla kisha kikafuatia kicheko kikubwa.’’
Pili, kuwa na matukio ya kiajabu. Ni matukio ambayo yapo tofauti na maisha halisi kwa mfano, mtu kutembeajuu ya maji bila kuzama ni tukio la kiajabu. Mwandishi amemuonyesha mhusika Mimi kutembea juu ya maji katika (uk. 15) kama mwandishi anaposema,
  “… hatukwenda sana kabla ya kutumbukia kwenye mto uliokuwa na maji mengi ajabu. Lakini hatukuzama badala yake tulielea juu juu. Mwenzangu alinishikilia na kwa kiasi fulani nikajihisi kama Petro aliyetembea juu ya maji.”  
Tatu, kuwepo hali za kushangaza na za kuogofya. Katika riwaya hii ya Bina - Adamu, hali ya kushngaza na kuogofya imejitokeza katika (uk. 22) mhusika “Mimi” anasema,
“Niliangalia mikono yangu. Ilikuwa ya mtu mzima, lakini vyanda vyake vilikuwa vya mtoto. Nilipigwa na mshangao mkubwa lakini nikagutuka kuwa nilipokuwa nikiishi kwa babu nilikuwa mtoto. Labda nilishaanza kukua lakini kwanini vyanda vyangu vilibakia kuwa vya mtoto mdogo?”
 Hali hii ya mtu mzima kurudi ni hali ya kushangaza na kuogofya. Vilevile mwandishi ametumia matukio ya ajabu kwa kuonyesha chakula na kinywaji kisichokwisha na chenye kushibisha mara moja. Katika (uk. 134) mwandishi anasema,
“nilichukua kile kibuyu changu na kukifungua kisha nikamnyooshea. Alikichukua bila ya kuuliza lolote akayapigamafunda kadhaa na kuyameza kwa sauti iliyoweza kusikika na hata mtu akiwa mbali.”
Baada ya kufafanua maana ya riwaya, dhamira chomozi zilizojitokeza katika riwaya ya Bina –Adamu, riwaya inayofanana na riwaya hii kimaudhui ni Mzingile ufuatao ni ufanano wa riwaya hizi kimaudhui.
 Matabaka na utabaka. Suala la matabaka limeweza kujadiliwa kwa kina sana katika riwaya ya Mzingile pia katika riwaya ya Bina – Adamu.Mwandishi wa riwaya ya Mzingile ameweza kuonesha matabaka ya kisiasa, kiuchumi hata kijamii. Mfano, msanii anaonesha tabaka la kisiasa kupitia kwa mhusika kipofu, ambaye ni tabaka tawaliwa lisilomiliki chochote na ambalo halina sauti juu ya tabaka tawala, halikadhalika Kipofu anatumika kama tabaka tawaliwa lisilo na elimu linaloongozwa na tabaka tawala lenye elimu (uk. 28) ambapo hadhira (watazamaji) wamekaa kulingana na hadhi zao. Mwandishi anaonesha jinsi tabaka tawala wanavyotumia mali kwa mambo ya starehe bila kujali wala kuwasaidia tabaka tawaliwa kwa kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili. Katika (uk. 45) mwandishi anasema,
“Katika mstari wa mbele kabisa walikuwa wamekaa wanasiasa mashuhuri kutoka               nchi mbalimbali kama kawaida yao hawakupenda kuona mtu mwingine mbele yao.              Viti vyao vilikuwa vya starehe zaidi. Walikuwa viongozi na walipaswa kuongoza                katika kuona. Nyuma yao walifuatia viongozi wa dini mbalimbali.”
Pia katika riwaya ya Bina-Adam matabaka yamejitokeza  kama ya kisiasa, kiuchumi, na kijamii.Pia utabaka katika jamii zetu limekuwa tatizo kubwa kwani tunaona viongozi wanajilimbikizia madaraka na kuwakandamiza wanyonge. Seuze ya hayo katika jamii yapo matabaka kati ya wenye navyo na wasio navyo, wasomi na wasio soma na madhara ya matabaka katika jamii yanaleta utengano baina ya wanajamii jambo ambalo sio zuri.
Usihiri, haya ni mambo ya ajabuajabu yasiyoweza kuthibitika na ambayo yapo kinyume na mambo ya uhalisia wa jamii.  Katika riwaya ya Mzingile usihiri umeweza kujitokeza kwa namna mbalimbali. Mfano usihiri juu ya kuzaliwa na kukua kwa Kakulu, mwandishi anaonesha jinsi  Kakulu anavyozaliwa akiwa mtu mzima, mwenye ndevu, badala ya kunyonya anataka ubuyu na kitendo cha kuongea akiwa tumboni kama inavyothibitika katika (uk. 1), mwandishi anasema,
“Wanakijiji walimpa jina la Kakulu  kwa sababu alizaliwa akiwa na ndevu tayari-  Kakulu, kakubwa, kazee! Habari zilivuma kwamba hakupata kunyonya ziwa la  mama yake. Siku hiyohiyo aliyozaliwa, alimwomba mama yake ubuyu ulioivia mtini.”
Halikadhalika suala la usihiri linajitokeza kwenye chemichemi, sehemu ambayo kichaa pamoja na kundi kubwa la watu wanapooga maji ya mvua na kujikuta wakibanduka na kubaki mifupa tu kisha wanakimbiana. Katika (uk. 20), mwandishi anasema,
               “Nilipojaribu kujisugua mwili nilibandua ngozi na nyama yake mifupa ya mikono                   yangu ilianza kuonekana sote tulikuwa mifupa iliyosimama na kutembea.”
Pia suala la usihiri limeonekana katika riwaya ya Bina - Adamu! ambapo wakati mwandishi ametumia wahusika wa ajabu ajabu mfano, Hanna ambaye alikuwa anabadilikabadilika mara kwa mara anafanana na watu mbalimbali.
Suala la usihiri kama alivyotumia mwandishi kwenye kazi yake ya Mzingile na Bina- Adamu! pia lina uhalisia katika jamii tunayoishi ikizingatiwa kuwa, kuna masuala ya ushirikina na uchawi mambo ambayo  yanayohusiana na kuwafanya watu misukule  ambao huwa hawaonekani katika macho ya kawaida ya binadamu. Pia usihiri hujitokeza katika jamii wananchi ambao wana migogoro ya nafsi kwani mgogoro ukikomaa mwishoni wanauana. Mfano, wanaua watoto waopamoja na ndugu zao.
Usihiri pia, unajidhihirisha katika jamii yetu ya sasa kwani,kuna mambo ya ajabu ajabu yanayojitokeza katika jamii yetu tuliyomo. Kwa mfano, wanajamii kusafiri kwa ungo, kusafiri kwa kumtumia myama fisi, pia kuwaroga watu usiku wakiwa wamelala.
Kwa kuhitimisha, tunaweza kusema kuwa riwaya ya Bina -Adamu inasawiri maisha na hali halisi ya kiafrika na dunia kwa ujumla. Kwa mfano, sera ya dunia ambayo ni utandawazi imeelezewa kwa urefu na undani zaidi kwa kuonyesha  madhara yake katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea.Vilevile inasawiri hali halisi kwa sababu katika jamii za kiafrika kuna watu ambao wanatafuta suluhisho kama ambavyo mhusika mkuu Mimi, ambaye alisafiri kwenda sehemu mbalimbali duniani kutafuta ufumbuzi juu ya maisha ya watu wa nchi za kiafrika. Hivyo nchi za kiafrika zikijaribu kutatua matatizo kwa mbinu tajwa kama ubaguzi wa rangi, ukabila na kufanya vitu vionekane kwa uhalisia wake (ukengeushi), zinaweza kupambana na matatizo mbalimbali.




MAREJELEO
12-07-wamitila- 1-pdf,Swahili forum (2005):95-97, mahojiano mafupi na cutz diegner juu ya
riwaya ya Bina –Adamu.
Florence L. V. (2013), Sifa za uhalisia ajabu na umuhimu wake katika utenzi wa mwana
Fatuma: tasnifu; chuo kikuu cha Nairobi.
Madumula J.S, (2009), Riwaya ya Kiswahili historia na misingi ya uchambuzi. NAIROBI:
Sitima printer and station ltd.
Muhando P.Balisidya (996), Fasihi sanaa za maonyesho. Dar es salaam Tanzania publishing
house.
Nkwera, F.V (1978), Sarufi na fasihi Sekondari na vyuo. Dar-es-salaam Tanzania Publishing
house.
Wamitila, K.W (2003), Kamusi ya fasihi, istilahi na nadharia.
www.GAFKO SOFT.com/swa/Riwaya 2009-2004


ANGALIZO: MAKOSA YALIYOJITOKEZA KATIKA MAKALA HII NI YA KIUCHAPAJI NA SIO YA VYANZO REJEWA HAPO JUU.



 

.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni